Showing posts with label HOME. Show all posts
Showing posts with label HOME. Show all posts

Thursday, 7 May 2015

JUA FAIDA YA ZAO LA MUHOGO KIUCHUMI

Zao la muhogo kwa wananchi walio wengi linachukuliwa kama la kinga dhidi ya njaa. Miaka ya hivi karibuni kumezuka teknolojia nzuri ya kufanya zao la muhogo litumike kwa usafi zaidi na hata kuwa zao la biashara zaidi jambo ambalo litawafanya wakulima wa Tanzania kuwafikia
Zao la muhogo
wakulima wa Afrika Magharibi ambao wameanza kusindika zao la muhogo kwa muda mrefu na kunufaika kiuchumi.
Utafiti uliofanyika nchini Italia kuhusiana na zao hilo unaonyesha kuwa muhogo unaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali zaidi ya 300 yakiwemo unga wa muhogo, tambi, biskuti, mafuta ya lishe, keki, sabuni ya
unga, kuni, mboga, pamoja na bidhaa nyingine nyingi.
Maofisa ugani wakieneza elimu ya kisasa ya kusindika muhogo katika maeneo mengi nchini miaka kumi ijayo, zao la muhogo litakuwa ni zao kubwa na lenye heshima katika kuinua uchumi na kipato cha mkulima kwa kulifanya kuwa zao la chakula na biashara.