Wednesday, 1 July 2015
MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO...2015-2016
KUANGALIA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA ELIMU YA "A LEVEL" FUNGUA HAPA
Wednesday, 13 May 2015
MILIMA MAARUFU TANZANIA.
Tanzania ni moja ya nchi ambayo imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi sana ikiwemo milima. na hutumiwa hizo rasilimali ikiwemo na milima kuweza kuwa ni chanzo kikubwa chakuleta pato la nchi kupitia utalii wa ndani na nje ya nchi. miongoni mwa milima ambayo ni mikubwa na maarufu Tanzania ni Kilimanjaro, udzungwa, Usambara, Ol doinyo lengai na Rungwe. si hiyo ipo mingine mingi isipokuwa hiyo ni baadhi ya milima ambayo nimaarufu zaidi.
Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ni maarufu duniani kutokana na mandhari nzuri ya Mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kuliko yote Afrika na inapatikana katika nchi ya Tanzania. Hifadhi hii ina ukubwa wa kilometa za mraba 755 na iko umbali wa kilometa 45 kutoka Moshi mjini. Kilele cha Kibo
chenye urefu wa mita 5895 (futi 19340) ndio kivutio kikubwa kwa wageni
kutoka ndani na nje ya nchi kutokana na kufunikwa na theluji.
Mlima huu ni moja kati ya milima ambayo kilele chake hufikiwa kwa
urahisi na hivyo kuwa kivutio kikubwa kwa wapanda milima kutoka kila
pande za dunia.
PICHA ZA MLIMA KILIMANJARO
Saturday, 9 May 2015
SHERIA YA MAKOSA YA MITANDAO,2015
Sheria hii ya makosa ya mtandao, 2015 imebainika kuwa na
mapungufu makubwa sana. Mapungufu hayo yamebainika kuwa, kama sheria ikipita yanaweza
kuifanya nchi ikawa ni kati nchi adui za matumizi ya mtandao wa Teknolojia ya Habari
na Mawasiliano duniani.
Watanzania wote wanatakiwa kufahamu kuwa muswada ukipita utatumika nchini kote yani Tanzania Bara na Visiwani. Watanzania waliowengi hawafahamu Sheria hii inawahusu kwa namna gani; lakini kwa lugha rahisi ni kuwa itamuathiri mtu yeyote anayeweza tumia mtandao wa intaneti kwa kutimia kifaa chochote iwe kompyuta kubwa au vifaa vyenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta kama Simu za mikononi,saa, televisheni na vifaa vingine vinavyoendana na hivyo.
Watanzania wote wanatakiwa kufahamu kuwa muswada ukipita utatumika nchini kote yani Tanzania Bara na Visiwani. Watanzania waliowengi hawafahamu Sheria hii inawahusu kwa namna gani; lakini kwa lugha rahisi ni kuwa itamuathiri mtu yeyote anayeweza tumia mtandao wa intaneti kwa kutimia kifaa chochote iwe kompyuta kubwa au vifaa vyenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta kama Simu za mikononi,saa, televisheni na vifaa vingine vinavyoendana na hivyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)

