Monday 13 July 2015

Mkuu wa Jeshi la Polisi Azungumzia Tukio La Majambazi Kuvamia Kituo Cha Polisi Jana.......Asema Waliouawa ni Polisi 4 na Wananchi 3



Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu akizungumza na waandishi wa habari leo katika kituo cha Stakishari Ukonga jijini Dar es Salaam, kutokana na Askari wa Jeshi la Polisi  na raia wa eneo hilo kuuwawa na majambazi waliovamia katika kituo hicho usiku wa kuamkia leo. 

Wednesday 13 May 2015

MILIMA MAARUFU TANZANIA.

Tanzania ni moja ya nchi ambayo imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi sana ikiwemo milima. na hutumiwa hizo rasilimali ikiwemo na milima kuweza kuwa ni chanzo kikubwa chakuleta pato la nchi kupitia utalii wa ndani na nje ya nchi. miongoni mwa milima ambayo ni mikubwa na maarufu Tanzania ni Kilimanjaro, udzungwa, Usambara, Ol doinyo lengai na Rungwe. si hiyo ipo mingine mingi isipokuwa hiyo ni baadhi ya milima ambayo nimaarufu zaidi.

Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ni maarufu duniani kutokana na mandhari nzuri ya Mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kuliko yote Afrika na inapatikana katika nchi ya Tanzania. Hifadhi hii ina ukubwa wa kilometa za mraba 755 na iko umbali wa kilometa 45 kutoka Moshi mjini. Kilele cha Kibo chenye urefu wa mita 5895 (futi 19340) ndio kivutio kikubwa kwa wageni kutoka ndani na nje ya nchi kutokana na kufunikwa na theluji.
Mlima huu ni moja kati ya milima ambayo kilele chake hufikiwa kwa urahisi na hivyo kuwa kivutio kikubwa kwa wapanda milima kutoka kila pande za dunia.

                        PICHA ZA MLIMA KILIMANJARO
 

Saturday 9 May 2015

SHERIA YA MAKOSA YA MITANDAO,2015

Sheria hii ya makosa ya mtandao, 2015 imebainika kuwa na mapungufu makubwa sana. Mapungufu hayo yamebainika kuwa, kama sheria ikipita yanaweza kuifanya nchi ikawa ni kati nchi adui za matumizi ya mtandao wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano duniani.

Watanzania wote wanatakiwa kufahamu kuwa muswada ukipita utatumika nchini kote yani Tanzania Bara na Visiwani. Watanzania waliowengi hawafahamu Sheria hii inawahusu kwa namna gani; lakini kwa lugha rahisi ni kuwa itamuathiri mtu yeyote anayeweza tumia mtandao wa intaneti kwa kutimia kifaa chochote iwe kompyuta kubwa au vifaa vyenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta kama Simu za mikononi,saa, televisheni na vifaa vingine vinavyoendana na hivyo.
                                                                               :ZAIDI SOMA HAPA:

Thursday 7 May 2015

TAMBUA MBUGA KUU TATU ZA WANYAMA TANZANIA

Tanzania imebarikiwa kwa wanyama wa kila aina. Kuna mbuga kubwa tatu ambazo Tanzania imehifadhi wanyama mwitu. Mbuga hizi ni Mikumi, Manyara na Serengeti. Mbuga hizi zinatunzwa na wafanya kazi wa wizara ya Utalii na Mali Asili,Tanzania. Wageni wengi wanapendelea kuja Tanzania kutembelea mbuga za wanyama na hivyo kujionea fahari yetu katika mbuga hizo. Pia kupitia mbuga hizo husaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza pato la taifa na hivyo kuendeleza nchi yetu kujisaidia katika huduma zake mbalimbali.

Hifadhi ya Mikumi ni moja ya hifadhi mashuhuri na kubwa nchini Tanzania. Eneo kuu na muhimu katika hifadhi hii ni uwanda wa mafuriko pamoja na safu za milima ambazo zinapatikanandani ya hifadhi hii. Mbuga za wazi ndizo zinazoshamiri katika uwanda wa mafuriko na kuishia katika misitu ya miombo inayofunika mabonde yaliyo chini ya hifadhi.
Twiga katika hifadhi ya mikumi

Hifadhi hii ina ukubwa wa kilometa 3230 na ipo umbali wa kilometa 283 magharibi mwa Dar ea Salaam. Aidha hifadhi hii iko kaskazini ya mbuga ya Selouse na iko njiani unapoelekea katika hifadhi ya Udzungwa, Selouse na Ruaha kwa barabara kutoka Dar ea Salaam na Inapatikana katika Mkoa wa Morogoro.

Hifadhi ya Serengeti ni eneo kubwa la mbuga na misitu katika Tanzania ya kaskazini hasa katika mikoa ya Mara na Arusha ikipakana na nchi ya Kenya.
Eneo lake ni 14,763 km² na kijiografia inaendelea ndani ya Kenya inapoitwa Hifadhi ya Masai Mara.
Kuna idadi kubwa ya wanyamapori. Serengeti pamoja na Masai Mara inajulikana hasa kwa uhamisho wa kila mwaka wa zaidi ya milioni moja ya nyumbu wanaovuka mto Mara. Kuna pia aina nyingi nyingine za wanyama, kati yao "watano wakubwa" wanaovuta watalii hasa yaani tembo, simba, chui, fisi, kifaru na nyati.

JUA FAIDA YA ZAO LA MUHOGO KIUCHUMI

Zao la muhogo kwa wananchi walio wengi linachukuliwa kama la kinga dhidi ya njaa. Miaka ya hivi karibuni kumezuka teknolojia nzuri ya kufanya zao la muhogo litumike kwa usafi zaidi na hata kuwa zao la biashara zaidi jambo ambalo litawafanya wakulima wa Tanzania kuwafikia
Zao la muhogo
wakulima wa Afrika Magharibi ambao wameanza kusindika zao la muhogo kwa muda mrefu na kunufaika kiuchumi.
Utafiti uliofanyika nchini Italia kuhusiana na zao hilo unaonyesha kuwa muhogo unaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali zaidi ya 300 yakiwemo unga wa muhogo, tambi, biskuti, mafuta ya lishe, keki, sabuni ya
unga, kuni, mboga, pamoja na bidhaa nyingine nyingi.
Maofisa ugani wakieneza elimu ya kisasa ya kusindika muhogo katika maeneo mengi nchini miaka kumi ijayo, zao la muhogo litakuwa ni zao kubwa na lenye heshima katika kuinua uchumi na kipato cha mkulima kwa kulifanya kuwa zao la chakula na biashara.

Sunday 22 February 2015

JE WAJUA HILI?... AU NDO WAJUZWA?

Ivi waijua korosho au waisikia? .....Watumia sana lakini ni baada ya kuikuta dukani imeshakwisha andaliwa....je, watambua mwanzo kabla ya kutengeneza na kuweka dukani teali kwa matumizi inafananaje?....
OOOOOOhhhh...sikia fahari leo hii kutambua kabla ya kuitumia hiyo korosho inatoka wapi..kwani ninahofu kwako,kuweza tu kuitamka na kuitumia pasina kutambua vipi inakuwa mwanzo kabla ya kukufikia.
Sasa kabla bado korosho haijawa korosho kutoka katika miti yake huanza kufanyiwa maandalizi ya mashamba ambayo miti hiyo hulimwa, na maandalizi hayo huanza tuu baada kuanza kutokeza maua ya zao hilo.
Mti wa mkorosho


Miti hii mpaka kufikia hatua ya kuzaa korosho huwa ina fanyiwa kharama mbalimbali kama kulimiwa na kupuliziwa dawa zaidi ya mara tatu na zaidi katika kipindi tofauti tofauti.

Baada ya maandalizi hayo huwa inasubiriwa kwakipindi fulani wakati huo kukiwa na maangalizi ya hali ya juu zidi ya wadudu waaribio maua ya korosho,

Ndipo baadae baada ya uangalizi na huduma mbalimbali huanza taratibu kutengeneza korosho mbichi ( ambazo huitwa madafu ya korosho),matunda (mabibo ya korosho) hatimaye kukauka na kuanza kuanguka kutoka mtini. ikifika hatua hyo sasa ndipo wakulima huanza kuokota korosho na kurudisha

Saturday 21 February 2015

TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUTUMA MAOMBI YA MAFUNZO YA STASHAHADA YA UALIMU KWA MWAKA WA MASOMO 2015

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi  (NACTE) linapenda kuwataarifu wananchi kuwa limeongeza muda wa kutuma maombi ya Mafunzo ya Stashahada ya Ualimu, awamu ya pili hadi tarehe 28 Februari  2015. Baada ya tarehe hiyo, majina ya waombaji watakaochaguliwa kujiunga na mafunzo ya Stashahada ya Ualimu awamu ya pili yatatangazwa mwanzoni mwa mwezi Machi 2015 kwenye tovuti ya Baraza ambayo inaonekana katika Tangazo hili.
Watu wote wenye sifa za kujiunga na mafunzo haya wanaombwa kuitumia fursa hii muhimu kama inavyoelekezwa kwenye tovuti ya Baraza:  Kwa maelezo zaidi bofya hapa.


Imetolewa na;

Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
Tarehe 10/2/2015

SERIKALI YAAHIDI KUAJILI WALIMUU WAPYA 35,000 MWAKA HUU

Waziri Mkuu Mizengo Pinda, amesema Serikali imepanga kuajiri walimu zaidi ya 35,000 kwa ajili ya shule za sekondari, ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu nchini.
Alitoa kauli hiyo jana jioni wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa kata ya Kiwere, baada ya kukagua ujenzi wa maabara na kuzindua nyumba nne za walimu kwenye Shule ya Sekondari ya Kiwere, tarafa ya Kalenga, wilayani Iringa.

 
Waziri Mkuu alisema walimu hao
watagawanywa kwenye shule kulingana na mahitaji yaliyokwishawasilishwa na   watakapopata mgawo wao, hawana budi kuangalia kwanza shule zenye miundombinu iliyokamilika kama ilivyo kwa shule hiyo.
Akifafanua kuhusu kasi ya ujenzi wa maabara, Waziri Mkuu alisema: “Mkoa mzima wa Iringa unahitaji maabara 318 na zilizo tayari mpaka sasa ni 108.
 
“Lakini kuna nyingine 141 ambazo zimekwishaanza kujengwa na zimefikia hatua nzuri. Nimeambiwa katika muda mfupi ujao kutakuwa na maabara 249

KUMBUKUMBU ZA VURUGU ZA GESI MTWARA


Hiki kilikua ni kipindi cha majonzi makubwa kwa wana mtwara katika sakata la kuhitaji haki yao. Ama hakika kwa wale wote tunaokumbuka kipindi hiki hatutamani kuhitajia kutokea tena kipindi kama hiki. Simanzi zilitawala kutokana na watu kuaribiwa makazi yao, na hata kukosa ndugu zao.Mungu awatakie kheri wote waliokakumbwa na kharika lile.

Zifuatazo ni baadhi ya picha ambazo huonyesha matukio mbalimbali ya kipindi kile:-

ONA FAHARI KUSINI YETU

Pande za kusini Tanzania inawakilishwa na mikoa ya Mtwara,Lindi na Ruvuma ikipakana na mikoa ya Nyanda za juu Kusini ambayo ni Mbeya, Iringa na Njombe . Hii ni mikoa maarufu ambayo hufahamika. Huwa inajipatia umaarufu sana  hususani katika kilimo kikubwa sana cha Biashara Tanzania cha Korosho, Kupitia kilimo hicho kimekua kikipatia pato serikali na hata kuwawezesha wanainchi waishio pande hizo kuendeshea maisha yao.

Hapa chini ni muonekano wa picha za Korosho na Mabibo yake.

Korosho na matunda yake.

Korosho zikiwa juu ya mti wake.
Hivi ndivyo ambavyo twajivunia nyumbani Kusini. Pamoja na shughuli si moja tuu. kuna nyingi na nyingi,miongoni mwa hizo ni shughuli za uvuvi ambazo hufanyika katika bahari ya Hindi, Pia kilimo cha Mahindi,Mihogo na hata Mtama. Hivy vyote hupatikana Maeneo haya ya kusini.

Pia Mikoa yetu hii imejaliwa kuwa na bandari kubwa miongoni mwa bandari zipatikanazo Tanzania, Na hata selous  ambayo hiyo hupatikana Liwale-lindi ikipakana na Mkoa wa Morogoro.
Pia ni fahari kwetu kutokana